Hatimaye Mpaka wa Ethiopia na Eritrea Wafunguliwa Baada ya Miaka 20

Hatimaye Mpaka wa Ethiopia na Eritrea Wafunguliwa Baada ya Miaka 20
Viongozi wa mataifa ya Ethiopia na Eritrea wameshuhudia kufunguliwa kwa mpaka huo muhimu ambao ulikuwa umefungwa kwa kipindi cha miaka 20 iliyopita kufuatia mzozo wa mpakani.

Hatua hiyo ni sehemu ya kuimarisha uhusiano kati ya mataifa hayo mawili, hali ambayo itaiwezesha Ethiopia kutumia bandari ya Assab.

Kituo kingine cha mpakani kilichopo karibu na mji wa Zalambessa nchini Ethiopia pia kinatarajiwa kufunguliwa hivi karibuni.

Mkataba wa amani uliyotiwa saini na waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed na Rais wa Eritrea Isaias Afwerki mwezi Julai umechangia kufufua uhausiano wa kidiplomasia na wa kibiashara.

Kufunguliwa kwa mpaka huo kunajiri wakati Ethiopia inasherehekea mwaka mpya.

Mapigano yaliyozuka katika eneo hilo la mpakani mnamo mwezi Mei mwaka 1998, yalisababisha vifo vya maelfu ya watu.

Hata hivyo mkataba huo haukutekelezwa kikamilifu baada ya Ethiopia kukataa kutekeleza uamuzi wa tume iliyobuniwa ya kusuluhisha mzozo huo wa mpakani


Eritrea ilijipatia uhuru wake kutoka kwa Ethiopia mwaka 1991 lakini jamaa za familia moja ziliendelea kuishi pande zote mbili za mpaka kati ya mataifa hayo mawili huku zikijivunia uhusiano mwema kati yao hadi mwaka 1998.

Yonas Fesseha, mkaazi wa Zalambessa ameiambia idhaa ya BBC Tigrinya kwamba anajiandaa kukutana tena kwa mara ya kwanza na mama yake pamoja na ndugu yake katika kipindi cha miaka ishirini.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad