Hatimaye Serikali ya Uganda Yamuachilia Bobi Wine Kusafiri Kwenda Marekani Kwaajili ya Matibabu

Hatimaye Serikali ya Uganda Yamuachilia Bobi Wine Kusafiri Kwenda Marekani Kwaajili ya Matibabu
Mbunge wa Uganda ambaye inadaiwa aliteswa na maafisa wa usalama, Robert Kyagulanyi  maarufu kwa jina la Bob Wine ameruhusiwa kusafiri kuelekea Marekani kwaajili ya matibabu.

Alhamisi usiku Polisi walimkamata Kyagulanyi na mbunge mwenzake wa upinzani Francis Zaake uwanja wa ndege wa Kampala wakati wakijiandaa kwenda nje ya nchi kupatiwa matibabu.

Polisi walidai kuwa viongozi hao wa upinzani, ambao wote wanakabiliwa na tuhuma za uhaini walikuwa katika harakati za kukimbia nchi.

Hata hivyo, wabunge hao wawili wamesema kuwa waliteswa baada ya kukamatwa huko nyuma na hospitali ya Kampala ilitoa pendekezo kwamba wapatiwe matibabu nje ya nchi.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad