Huyu Hapa Askari Mwanamke Aliyezuia Mauaji ya WhatsApp

Askari mwanamke India aliyezuia Mauaji ya WhatsApp
Polisi waliamua kufanya uchunguzi kwenye simu za wanavijiji waligundua kuwa kati ya video na picha 30 na 35 ambayo iliwakuwa ikisambazwa na kumuonesha mtoto akiwa ametekwa,kwa uhalisia, hiyo ilikuwa ni kutoka katika moja ya filamu kutoka nchini Pakstani ambayo iliondolewa baadhi ya maudhui yake na kisha kufuatiwa na sauti.

Jambo lisilo la kawaida latokea muda wa magharibi kwa wanavijiji zaida ya 400 katika mji wa Telangana uliopo kusini mwa India

Wanaume na wanawake walirejea majumbani mwao mapema kuliko kawaida kutoka mashambani,wakifunga milango,wakizima taa na kusalia ndani licha ya watoto kuwa na kawaida ya kucheza nje kwa muda mrefu, tulikuwa wa kwanza kurudi,mitaa yote ilikuwa kimya na hofu ikiendelea kutanda.

Hii ilikuwa si tabia ya kawaida kwa majira ya kiangazi kwa wanavijiji wengi kulala nje ya nyumba zao kwenye vitanda vya Kamba vilivyokuwa uani.

Mwezi Machi askari wa kijijini ambapo kulikuwa na askari zaidi 4,000 waliokuwa waliokuwa wakifanya uchunguzi juu ya tabia hii mpya isiyokuwa ya kawaida kwa wanavijiji hao.

Wakati akirejea katika wilaya ya Gadwal, Mkuu wa police wa wilaya Rema Rajeshwari,alimsikiliza afisa wa police mwenye cheo cha konstebo bila ya kumuelewa.

Katika kichwa cha habari kwenye WhatsApp yenye taarifa isiyo ya kweli.

"Walisema maisha ya vijijini yalikuwa ya mashaka baada ya magharibi,wakisema hawajawahi kuona kitu kisichokuwa cha kawaida kwao hapo kabla," Bi Rajeshwari aliniambia.

Siku chache baadaye polisi walijaribu kufanya uchunguzi wa nini kilichotokea, lakini walichogundua ni mwanga wa nyota tu,baada ya wanavijiji kuona video na sauti iliyorekodiwa ikisambazwa katika mtandao wa WhatsApp na kuzusha taharuki kwao.

Kulikuwa na hofu kubwa baada ya video na sauti hiyo iliyorekodiwa kwa lugha ya wenyeji ya Telugu ikimuonesha mtu akitoa viungo vya ndani vya binadamu, na sauti ya mwanaume mmoja ikisema kuwa ni kundi la wahalifu wa mtaani kwa miongo kadhaa ambao wamekuwa wakifanya uhalifu kwa kutoa viungo vya ndani vya bianadamu.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad