Huyu ndiye mgeni rasmi mechi kati ya Yanga na Simba kesho


Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limemtangaza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, kuwa mgeni rasmi katika mchezo wa Simba na Yanga utakaopigwa kesho Uwanja wa Taifa. 

Simba na Yanga zinashuka dimbani kesho Septemba 30 2018 kuendeleza safari ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Bara ukiwa ni mchezo wa kwanza kwa timu hizo mbili msimu huu. 

Ndugai ameitikia wito wa TFF na amekubali kuhudhuria mchezo huo ambao utaanza majira ya saa 11 jioni. 

Kuelekea mechi hiyo, TFF kupitia Ofisa Habari wake, Clifford Mario Ndimbo, amesema hali ya usalama itakuwepo kutokana na vyombo husika kuwahakikishia kutokuwepo kwa vurugu yoyote ile. 

Simba inaenda kucheza na Yanga ikiwa na kumbukumbu katika mchezo wa mwisho walipokutana na watani zao msimu uliopita kwa bao 1-0.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad