Jack Wolper 'Mimi nina Pepo la Kuwachukia Ma Ex Wangu..Hadi Nilikosa Deal Kubwa'


Msanii wa filamu za Bongo Movie na mjasiriamali Diva Jacqueline Wolper ameibukana kudai kuwa katika Mahusiano yake yote ambayo amewahi kuwa nayo wanaume anaoachana nao bado wanakuwa wanampenda.

Wolper amefunguka kuwa katika maisha yake yote anapokuwa anaachana na wanaume aliokuwa nao Kwenye Mahusiano wote wanakuwa bado wanamuhitaji licha ya yeye kuwatema na kutowahitaji tena.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Wolper ambaye ameshawahi kuwa Kwenye Mahusiano na mastaa kadhaa Bongo ikiwemo staa wa Bongo fleva Harmonize amefunguka:

Ujue mimi kila nikiachana na mwanaume anakuwa bado ananipenda, pale nilikimbia kwa sababu nikiachana na boyfriend, huwa sipendi niendelee kuwasiliana naye wala kusogeleana naye, sipendi kusalimiana na X.

Ilishawahi kutokea X ananihitaji kwa ajili ya mambo ya kibiashara lakini kwa sababu nakuwa sihitaji kabisa kuwasiliana nao nili-crash halafu nikakosa dili, hilo ni pepo ambalo ninalo nadhani nitamwambia mchungaji aniombee”.

Lakini pia alizungumzia sakata la kutemwa kama jaji wa shindano la Miss Lake Zone na amedai kuwa waandaji wa shindano hilo walitumia jina lake kutafutia kiki baada ya Shindano lao kubuma.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad