Kagame Awaachia Huru Mkosoaji Wake na Aliyepanga Kumuua


Kagame


Serikali ya Rwanda imemuachia huru aliyekuwa mkosoaji mkuu wa Rais Paul Kagame, ambaye alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 15 jela kwa kosa la kuhatarisha amani.

Victoire Ingabire, ametajwa kuwa miongoni mwa wafungwa 2,141 walioachiwa huru kupitia msamaha wa rais uliotangazwa wiki hii.

Mwanamke huyo aliyekuwa akimkosoa Rais Kagame, amekuwa akidai kupitia wawakilishi wake kuwa kifungo chake kilikuwa na shinikizo la kisiasa

Baada ya kutoka jela, Ingabire alimshukuru Rais Paul Kagame na kudai kuwa ni mwanzo mzuri wa kufungua uwanja wa siasa nchini humo.



Victoire Ingabire

Hata hivyo, Waziri wa Sheria, Johnston Businge alikanusha taarifa kuwa mwanamke huyo alifungwa kwa shinikizo la kisiasa.

“Kuachiwa kwake hakuna uhusiano wowote na siasa, na kufungwa kwake hakukuwa na uhusiano wowote na siasa,” alisema Businge.

Ingabire alikamatwa baada ya kurejea kutoka uhamishoni nchini Netherlands akiwa kwenye mpango wa kugombea urais. Alizuiwa kugombea urais kutokana na tuhuma zilizokuwa zinamkabili na baadaye alipatikana na hatia na kufungwa jela.



Kizito Mihigo

Atiwa mbaroni kutoa ofa vinywaji vyenye vilevi na kubaka wadada Dar, Mwanza, Arusha
Katika hatua nyingine, jina la mwimbaji maarufu, Kizito Mihigo aliyekuwa anatumikia kifungo cha miaka 10 jela kwa kosa la kupanga njama za kumuua Rais Kagame.

Madam Rita aanika wanachowafanyia washiriki wa BSS nyuma ya pazia
Kuachiwa huru kwa Mihigo kumekuja wiki moja baada ya kuwasilisha barua ya kuahirisha rufaa ya kupinga hukumu yake.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad