Kama Hauna Tiketi Marufuku Kuonekana Taifa Kesho- TFF

Kama Hauna Tiketi Marufuku Kuonekana Taifa Kesho- TFF
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema hakuna mtu yeyote atakayeruhusiwa kukatisha ukuta wa Uwanja wa Taifa kesho Jumapili kama atakuwa hana tiketi ya kuingilia uwanjani.



Simba na Yanga kesho ndiyo mara ya kwanza watakutana katika msimu huu wa 2018/19 mch­ezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam saa 11 jioni.



TFF imefanya hivyo ili kuimarisha ulinzi na kuzuia fujo zote ambazo zinaweza kuhatarisha usalama wamashabiki watakaojitokeza uwanjani hapo kesho.


Kikosi cha timu ya Simba.

Ofisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo alisema kuwa tiketi zitaendelea kuuzwa lakini mwisho itakuwa ni leo Jumamosi na kesho hakutakuwa na uuzwaji katika eneo la Uwanja, lengo ni kuimari­sha ulinzi kwa mashabiki ambao watajitokeza uwanjani hapo kushuhu­dia mchezo huo.



“Kumekuwa na vikao mbalimbali kuhakikisha mchezo huu unakuwa salama kwa kuhakikisha tunaimarisha ulinzi kama inavyofahamika kuwa ni moja ya michezo inay­okusanya watu wengi zaidi.


Kikosi cha timu ya Yanga.

“Na mtu yeyote am­baye atakuwa hana tiketi basi siku ya Jumapili asikatize katika ukuta wa uwanja kwani kutakuwa na ulinzi wa kutosha ku­hakikisha watu wanaoku­ja hawapati bugudha yeyote,” alisema Ndimbo. Mpaka jana tiketi 1300 zilikuwa zimeuzwa.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad