Kilichomfanya Irene Uwoya na Tausi wakamatwe na Polisi Mbeya

Moja kati ya stori zilizosambaa katika mitandao ya kijamii leo kuhusiana na muigizaji Irene Uwoya ni stori ya kudaiwa kuwa alikamatwa na Polisi jijini Mbeya na kulazwa katika kituo cha Polisi Mbeya Mjini.

Irene na baadhi ya wasanii wengine akidaiwa kuwemo Mtanga na Tausi walikamatwa usiku wa Jumamosi ya September 22 kuamkia September 23 baada ya kukutwa Bar Mbeya wakiwa wamevuka muda wa bar kufungwa.

Kwa kawaida Bar inatakiwa kufungwa saa sita usiku ila wao walikamatwa na Polisi wakiwa wamevuka muda huo, kitu ambacho kiliwafanya walale ndani na kutolewa kwa dhamana jioni ya September 23, AyoTV imeongea na Fadhili Atiki ambaye ndio muandaaji wa shughuli ya “Mimi Nimefurahi”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad