Kisa Mimba Kuchoropoka Chuchu Hans Awatolea Povu

Kisa Mimba Kuchoropoka Chuchu Hans Awatolea Povu
MWIGIZAJI wa kit­ambo kwenye tasnia ya filamu za Kibongo, Chu­chu Hans ametoa povu baada ya kudaiwa kuwa alinasa ujauzito ukachoropoka akiwa nchi­ni Afrika Kusini na mzazi mwenzie ambaye ni staa wa filamu, Vincent Kigosi ‘Ray’. Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Chuchu alisema anawashangaa wa­naomfuatilia kila kukicha. Alisema ni ajabu kuona watu wanamfuatilia kama ana mimba au la.

“Kila kukicha watu wanapenda ku­fuatilia mambo yangu na sijui ni kwa nini maana hata kama nikizaa watoto kumi na Ray, ni sawa kwa sababu ni mwanaume na ananipenda na kujali, kwa hiyo hata kama imetoka nitabeba tena hivi karibuni,” alisema Chuchu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad