Majambazi Wavamia Kijiji na Kuiba Mali Yenye Thamani ya Zaidi ya Sh3 Million

Majambazi Wavamia Kijiji na Kuiba Mali Yenye Thamani ya Zaidi ya Sh3 MillionI.
Watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wamemvamia mfanyabiashara, Burugu Mahanghija (44), mkazi wa Kijiji na Kata ya Lyabukande Shinyanga vijijini na kumpora fedha taslimu na mali yenye thamani ya zaidi ya Sh3 millionI.

Diwani wa Kata hiyo ya Lyabukande Joseph Misri, amesema baada ya kupora fedha na mali katika duka hilo, watuhumiwa hao waliwavamia wananchi wengine waliokuwa wakiangalia taarifa ya habari katika moja ya baa za eneo hilo na kuwapiga huku wakiwapora fedha na simu.

“Kelele za kuomba msaada ziliwafanya watuhumiwa hao waliokuwa na silaha kufyatua risasi hewani kutishia wananchi kabla ya kutokomea gizani,” amesema Misri.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad