Mama Mobetto Afungukia Wimbo Wa Mwanaye

Mama Mobetto Afungukia Wimbo Wa Mwanaye
Mama mzazi wa Mwanamitindo Hamisa Mobetto, Shufaa Rutiginga amefunguka kuhusu wimbo mpyawa binti yake ‘Madam Hero’ ambao ameshitiki Kwenye video.

Mama Mobetto amefunguka kuwa ameamua kuigiza kama mama kwenye wimbo wa kwanza wa mwanaye huyo wa Madam Hero kwa ajili ya kuweka baraka zake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na  Ijumaa Wikienda, Mama Mobetto amesema kwamba hakuna jambo linalompa faraja kama kuona wimbo huo wa mwanaye unaongoza kwa sababu alipoamua kuigiza kama mama kwenye wimbo huo ilikuwa ni kuubariki ili ufanye vizuri.

Alichokuwa anakitaka mwanangu ni baraka pekee kutoka kwangu kama mzazi na hilo limefanikiwa kwa kiasi kikubwa”.

Wimbo mpya wa Mobetto umeendelea kufanya vizuri kwa kushika chati ya juu Kwenye mtandao wa Youtube.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad