Mbelgiji Simba Ampa Maagizo Magumu Masoud Djuma Mechi yao Dhidi ya Yanga

Mbelgiji Simba Ampa Maagizo Haya Masoud Djuma
Kocha Mbelgiji wa Simba, Patrick Aussems, amefunguka juu ya maagizo aliyompa Msaidizi wake, Masoud Djuma kuhusiana na mechi dhidi ya watani wao wa jadi Yanga itakayopigwa Septemba 30 2018.

Aussems ameeleza kuwa Djuma alibakia jijini Dar es Salaam kuitazama Yanga ikicheza na Coastal Union ili kujua mbinu za kuimaliza kiulaini kuelekea mechi dhidi yao.

Mbelgiji huyo ambaye alishindwa kutamba mbele ya Mbao kwa kuambulia kichapo cha bao 1-0 amefunguka kumwacha Djuma Dar es Salaam kwa sababu anaifahamu Yanga vizuri kitu ambacho kitaisaidia Simba kujiandaa vizuri.

Kuelekea mechi hiyo Simba hawatocheza mchezo wao dhidi ya Biashara United uliokuwa umepangwa kupigwa Septemba 27 na Yanga kucheza Septemba 26 dhidi ya JKT Tanzania ili kuzipa timu hizo nafasi ya kujiandaa vema.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad