Nandy Afunguka Kuhusu Kuacha Kufanya Muziki

Nandy Afunguka Kuhusu Kuacha Kufanya Muziki
Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania Faustina Charles Mfinanga alimaarufu Nandy amefunguka mwanzo mwisho kuhusu malengo yake ya kuachana na mziki na kuhamishia nguvu zake kwenye biashara


Nandy ameongea hayo leo katika kituo cha habari cha Clouds Fm kwenye kipindi cha Leo tena na kusema  kuwa Bado miaka mitatu kuachana na muziki ” Mimi katika ndoto zangu ni kuwa mfanya biashara mkubwa sana na hata naanza kufanya muziki nilijiwekea malengo baada ya miaka mitano nitaacha muziki na niendeleze biashara zangu na hadi sasa nimeitumia miaka miwili tu 2016,na 2017 na mwaka 2020 ndio nitaacha muziki na sio kuwa nitakuwa sitoi ngoma hapana nitakuwa natoa ila kwa mwaka hata mara moja pia kuhusu show naweza kuwa nafanya kwa mwaka mara moja ili nipate muda wa kusimamia baishara zangu”



Nandy ni kati ya wanamuziki wa kike kutoka Tanzania wanao fanya vizuri kwa sasa akitambulishwa na ngoma yake ya Ninogeshe.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad