Serikali Kutoa 500,000 kwa Mwili Utakaotambuliwa

Serikali Kutoa 500,000 kwa Mwili Utakaotambuliwa
Miili 116 kati ya yote iliyoopolewa baada ya kuzama kwa Kivuko cha MV Nyerere juzi Septemba 20, 2018 imetambuliwa na ndugu.

Ndugu, jamaa na wananchi wamepiga kambi eneo la bandari ya Bwisya kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe tangu kazi ya uokoaji ilipoanza.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 22, mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amesema Serikali itatoa ubani wa Sh500, 000 kwa familia, kwa kila maiti itakayotambuliwa na kuchukuliwa kwa ajili ya maziko.

Tangu asubuhi leo, miili 30 imeopolewa na kufanya idadi ya miili iliyoopolewa hadi sasa kufikia 166 baada ya mili mingine 136 kuopolewa hadi jana jioni.

Miili yote iliyoopolewa imehifadhiwa katika Kituo cha afya cha Bwisya.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad