Tsunami Yaua Watu 380 na Wengine Kujeruhiwa Indonesia

Tsunami Yaua Watu 380 na Wengine Kujeruhiwa Indonesia
Watu zaidi ya 380 wamethibitishwa kufa baada ya tsunami kusababisha tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa richa 7.5 lilopiga mji wa Indonesia hapo jana.

Upepo mkali ulivuma kutoka Palu katika kisiwa cha Sulewesi kwa mita 3.

Video inayoonekana kwenye mitandao ya kijamii inaonyesha jinsi watu walivyokuwa wakipiga kelele huku wakikimbia kwa hofu.

Baada ya mshtuko wa tetemeko hilo, maelfu walizimia majumbani kwao na wengine wakielekea hospitalini ,hotelini na kwenye maduka makubwa.

Jitihada za uokoaji zinaendelea ingawa zimepata changamoto ya umeme kuwa umekatika.Njia kuu ya Palu imefungwa kutokana na daraja kuu kuanguka pia.

Mamlaka ya maafa nchini Indonesia imesema, watu wapatao 384 wamekufa ingawa idadi inategemewa kuongezeka na watu 540 wamejeruhiwa.

Miili mingi ilikutwa ufukweni kwa sababu ya tsunami lakini idadi yake bado haijafahamika.

Msemaji wa serikali ,Sutopo Purwo Nugroho aliiambia Reuters kuwa wakati onyo lilipotolewa hapo jana watu waliendelea na shughuli zao ufukweni na hawakuchukua tahadhari ya kukimbia mara moja hivyo wakawa miongoni mwa wahanga.

Wengine waliokoka kwa kupandia katika miti ili kukimbia upepo mkali.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad