Uwoya ashambuliwa baada ya Dogo Janja kuumwa


Muigizaji wa Filamu nchini Irene Uwoya, ambaye ni Mke wa Dogo Janja ameshambuliwa vikali na
Baadhi ya mashabiki katika mtandao wa Instagram  baada ya kutokuonekana maeneo ya hospitalini ambapo amelazwa mume wake Dogo Janja.

Dogo janja ambaye amesherekea siku yake ya kuzaliwa hapo jana Septemba 15,2018 akiwa amelazwa katika moja ya  hospitali maeneo ya Sinza, anasumbuliwa na tatizo la kupungukiwa na maji, kupumua kwa shida, kifua huku akisaidiwa na mashine ya kupumulia.

"Mpaka sasa hakuna watu wanaojuwa kama naumwa zaidi ya watu wangu wa karibu, ila naomba watu wangu na mashabiki waniombee, sitamani kulala hapa nataka na mimi nikasherekee birthday yangu hata Kama nikiwa nyumbani"Amesema dogo janja.

Mashabiki hao wameandika;
nakupasha_ubadilike Mda mwngn mjal na mmeo HV mmeo anaumwa unapata kbx ngv za kupost picha lol @ireneuwoya8

zamaradimyqueen Iv we dada unajckiaje ku post pc kama iz uko happy mumeo kalazwa anaumwa

tzalexis_mHaty  uwez jua labda hap yupo nje ya hospital sema hakutak mtu hajue..lakn wap mme wako huwez ficha watu waone kam umemtembelea badilika

mapishii Dada mwenye nyota ya kifo... dogo janja angemuuliza ndiku jomon doh masikin janja wa watu anapumulia oxygen mkewe yupo tuu mtaan.

Licha ya Dogo Janja kusema kwamba mke wake Irene Uwoya alikuwepo hospitalini hapo lakini hadi sasa kupitia mtandao wa instagram mashabiki wameendelea kumshambulia  Uwoya.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad