Zitto Kabwe Acharuka "Serikali itoe idadi Kamili ya watu Waliokuwa Kwenye MV Nyerere"


 Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Zitto Kabwe ametoa wito kwa serikali nchini Tanzania kutoa taarifa rasmi kuhusu idadi ya watu waliokuwa kwenye MV Nyerere ilipozama.

Bw Kabwe, ambaye ni mbunge wa Kigoma-Ujiji amesema ukosefu wa habari kuhusu idadi kamili ni dalili za ubaya wa sheria mpya ya takwimu nchini humo.

"Baadhi ya Watu wanasema kivuko kilikuwa na abiria kati ya 150 na 500. Ni muhimu Serikali itoe Taarifa rasmi ya idadi ya abiria waliokuwamo ili kuondoa sintofahamu ama Serikali iahidi kutoshtaki raia yeyote shuhuda kutoa makadirio ya Watu ili kuimarisha juhudi za uokoaji," amesema.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad