Baada ya Kutemwa Simba Djuma Apata Shavu Timu ya Ligi Kuu ya Rwanda


Aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Klabu ya Simba, Masoud Djuma amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuifundisha AS Kigali inayocheza Ligi Kuu ya Rwanda kuchukua nafasi ya Eric Nshimiyimana ambaye amejiuzulu kuifundisha klabu hiyo. 



Djuma ameondoka Simba baada ya kuwa kocha msaidizi kwa takribani mwaka mmoja lakini hivi karibuni ilitoka taarifa kuwa pande zote mbili zilikubaliana kuvunja mkataba. 



Kabla ya kujiunga na Simba, Djuma alikuwa kocha mkuu wa Rayon Sports ya Rwanda na aliondoka akiwa ameipa ubingwa wa Rwanda 2016/17. 



Amepata kazi fasta baada ya kurejea Rwanda huenda kwa sababu ya kufanya vizuri kwenye ligi kabla hajaondoka lakini pia uzoefu wake kwenye ligi hiyo kwa maana anajua afanye nini ili AS Kigali ifanye vizuri.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad