Hali ya Kimara Inatisha Abiria Wapandia Dirishani Wengine Wazimia

Hali ya Kimara Inatisha Abiria Wapandia Dirishani Wengine Wazimia
Changamoto ya usafiri wa mabasi yaaendayo haraka (UDART) kutoka maeneo ya Kimara kuelekea katikati ya Jiji la Dar es Salaam imeendelea kuwakabili wakazi wa Kimara na Mbezi kutokana na mabasi hayo kuwa machache.


Kwa takribani siku tatu sasa, mabasi hayo yameshindwa kukidhi huduma hiyo kwa watumiaji wa usafiri huo hali inayosababisha msongamano mkubwa kwenye kituo cha mabasi hayo Kimara.


Mapema leo Oktoba 10 kituo cha Kimara kimeonekana kuwa mlundikanao wa watu wengi hadi kusababisha baadhi ya abiria kuzirai kwa kukosa hewa ya kutosha huku wengine wakigombania kwa kupita dirishani mara yanapotokea.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad