Huyu Ndie Steve Mchumba Mpya Anayemzuzua Gigy Money Mpaka Amejichora Tatoo yake

Siku kadhaa nyuma zilizopita mwanadada Gigy Money alionekana akichora tatoo mpya katika maeneo ya kiunoni na kila mmoja kutaka kujua je tatoo hiyo inamuhusu nani, kwa habari za kunyapa nyapia ni kwamba kwa sasa gigy money yuko na mpenzi mpya .

Mwanaume huyo anaejulikana kwa jina la Steve ndie alieteka moyo wa Gigy money  mpaka kumfanya mwanadada huyo kuamua kuchoara tatoo yenye jina hilo.

Hata hivyo mwanadada huyo ambae alikuwa katika mahaba mazito na mwanahabari Mo jay  huku penzi hilo kupitia misukosuko mpaka kufikia hatua ya kupata mtoto mmoja wa kike kwa sasa limekufa na wawili hao hawako pamoja tena.

Pamoja na yote yanayoendelea ni kwa upande wa Gigy money ndio amekuwa msemaji mkuu huku Mo jay akijiweka kando na kuhusishwa na kitu chochote katika kufa kwa mahusiano yao.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad