Mama Kanumba: Nipo Tayari Kuhudhuria Harusi ya Lulu Endapo Nitaalikwa

Mama Kanumba: Nipo Tayari Kuhudhuria Harusi ya Lulu Endapo Nitaalikwa
Mama mzazi wa aliyekuwa Msanii wa Bongo movie Steven Kanumba, Florah Mtegoa maarufu kama Mama Kanumba amefunguka na kusema yuko tayari kuhudhuria harusi Lulu endapo ataalikwa.

Mama Kanumba ambaye aliweka wazi chuki yake dhidi ya Lulu baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia Marehemu Steven Kanumba ambapo alihukumiwa miaka miwili jela.

Mama Kanumba alifurahi baada ya kifungo cha Lulu lakini hivi sasa baada ya Lulu kuachiwa huru Mama Kanumba anafunguka na kusema wazi wazi kuwa hana chuki na Lulu na endapo ataalikwa Kwenye Harusi basi hatasita Kuhudhuria kwani hana kinyongo na Mrembo huyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha televisheni cha East Africa, Mama Kanumba alifunguka haya:

Hapa duniani sina chuki kabisa na Lulu na mimi akili yangu kwa hivi sasa akili yangu imeegemea upande mmoja tu nao ni kumuomba Mungu tu maana yeye ndio anatoa haki sawa kwa tajiri na hata masikini pia”.

Lulu alivalishwa pete na mpenzi wake ambaye ni CEO wa EFM Majizzo ambapo ndoa yake inatarajiwa kufanyika Miezi ya mbeleni.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad