Mapromoko ya ardhi Uganda Yaua Zaidi ya Watu 50

Mapromoko ya ardhi Uganda Yaua Zaidi ya Watu 50
Zaidi watu 50 wamepoteza maisha kutokana na maporoko ya ardhi na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa inayoendelea kunyesha mashariki mwa Uganda.

Mamia ya watu bado hawajulikani walipo huku maafisa katika wilaya ya Bududa wakihofu kuwa idadi ya waliopoteza maisha huenda ikaongezeka.

Walioshuhudia mkasa huo wanasema kuwa mwamba ulidondoka mtoni na kupasua kingo za mto hali iliyosababisha maji yaliyochanganyikana na matope kuanza kusomba watu vijijini.

Serikali imesema vikosi vya uokoaji vimepelekwa katika eneo hilo karibu na mpaka wa Uganda na Kenya lakini miundo mbinu ya barabara na daraja iliyoharibiwa imelemaza shughuli za uokozi.

Picha kutoka eneo la tukio zinaonyesha watu wakitoa miili kutoka ndani ya tope na kuweka kando

Maporomoko mengine ya odongo yalishuhudiwa katika eneo hilo la Bududa yalisababisha vifo vya zaidi ya watu 300 mwaka 2010.

Mwanamke ajioa nchini Uganda

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad