Mkuu wa Wilaya Bunda Ampigia Magoti Mtendaji wa Kata

Mkuu wa Wilaya Bunda Ampigia Magoti Mtendaji wa Kata
MKUU wa Wilaya, Lydia Bupilipili anadaiwa jana Oktoba 2, 2018 alimpigisha magoti Ofisa Mtendaji wa Kata ya Chitengule, Deus Kuliga alipokuwa akitoa taarifa ya kwa nini baadhi ya watendaji wa vijiji walishindwa kuhudhuria kikaoni.



Ofisa Mtendaji huyo alionekana kuwatetea viongozi hao kuwa walichelewa kupata taarifa na ndipo DC Bipilipili alipomwamuru kupiga magoti kwa kuwa ofisa huyo ndio alikuwa na jukumu la kuwapa taarifa viongozi wake.



Kwa upande wake Kulinga alisema; “Taratibu za kazi zifuatwe na mimi nipo tayari kujiuzulu lakini sipo tayari kudhalilishwa kama hivi utadhani nimeiba au nimetumia mali ya Serikali vibaya, Rais aangalie hali kama hizi”



“Mimi nina miaka zaidi ya 50, watoto 9 na wajukuu, kitendo cha kupigishwa magoti mbele ya kundi la viongozi wenzangu kama mtoto wa darasa la pili ni kunidhalilisha na hadi sasa sipo sawa,” alisema Kulinga.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. I just can't do it anyway.It's better to be fired than kneeling down in front of everybody.


    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad