Mkuu wa zamani wa Alshabaab wania Uongozi Serikalini Somalia

Aliyekuwa kiongozi wa kundi la wanamgambo wa kiislamu nchini Somalia, Alshababaab ametangaza kuwa anawania uongozi serikalini.

Mukhtaar Roobow anayefahamika pia kama Abu Mansur, alijitoa katika kundi la Alshabaab mnamo 2012 lakini alijisalimisha kwa serikali ya Somalia mnamo Agosti mwaka jana.

Atawania urais wa jimbo la ksuini magharibi mwa Somalia katika uchaguzi wa kieneo mwezi ujao.

 Mukhtar Robow amesema uamuzi huo kuingia katika siasa ni kufuatia wito wa wananchi, wafuasi wake katika jimbo hilo la kusini magharibi.

Amedhihirisha kwamba yupo tayari iwapo atashinda, kuidhinisha uhusiano thabiti na serikali ya shirikisho katika mji mkuu Mogadishu, ambayo imekuwa katika mzozo na tawala za baadhi ya majimbo.

Mukhtaar Roobow ni kiongozi wa juu zaidi katika kundi la al-Shabab kuwahi kujitoa kutoka kundi hilo na kujisalimisha, licha ya kuwa mojawapo ya waasisi wa kundi hilo.

Mwandishi wa BBC Bashkas Jugosdaay anasema kuna mgawanyiko.

Kuna kundi linalomtazama na sura ya uovu unaotekelezwa na Alshabaab uliochangia vifo vya maelfu ya watu.

Hilo ni donda ambalo daima kovu yake itasalia na kwa hivyo huenda ikawa vigumu kwake kupata uungwaji mkono kikamilifu.

Na kuna upande wa pili ambao wanatazama faida inayotokana na kujisalimisha kwake na kutoa ushirikiano kwa serikali kuu ya Somalia katika kusaidia kupambana na kundi hilo la wapiganaji wa kiislamu.

Hivyobasi matumiani ni kwamba huenda faida ikaongezeka na pengine ndio anastahili kupata uongozi huo. Na kama anavyoeleza mwenyewe Roobow, wapo watu waliomshinikiza kuwania uongozi, pengine ndio hakikisho la uungwaji mkono wake.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad