Nai na Fahyma Waingia Vitani Kisa Jina

Nai na Fahyma Waingia Vitani Kisa Jina
Mzazi mwenzake na staa wa Bongo fleva kutoka WCB Rayvanny, Fahyma amejikuta ndani ya bifu zito na Video vixen Maarufu kama Nai kisa Jina la Tanzania Baby.

Sakata hilo lilitokea siku chache zilizopita baada ya Nai kudai Fahyma amemuibia Jina lake la Tanzania Baby ambalo amekuwa akijiita tangu mwaka 2016 na kushangazwa na Fahyma kujiita hivyo hivi sasa.


Kwenye mahojiano aliyofanya na gazeti la Ijumaa, Nai alisema anashangaa kumuona Fahyma akijiita hilo jina la Tanzanian Baby wakati watu wote wanajua ni yeye hivyo aache kujisumbua kwa kutaka jina ambalo si lake.

Mimi nilianza kujiita Tanzanian Baby tangu mwaka 2016 nilipoanza tu kufanya u-video Vixen na kila mtu analijua hilo, sasa yeye kaanza kujiita juzi tu baada ya kuona Diamond kaliimba hilo jina kwenye wimbo wake wa ‘Eneka’ halafu namshangaa jinsi anavyopaniki vitu visivyokuwa na maana, atulize shobo mimi ndiyo Tanzanian Baby“.

Hii sio vita ya kwanza kutokea Mtandaoni baina ya warembo kisa jina wiki chache zilizopita tu tulishuhudia vita kati ya Wema Sepetu na Hamisa Mobetto kisa jina la Tanzania Sweetheart.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad