Nay wa Mitego Ashangwazwa na Simu ya Basata

Nay wa Mitego na Kiongozi wa Basata
Msanii nay wa mitego amezungumzia furaha yake hasa pale anapoona kuwa wimbo wake mpya uliotoka hivi karubuni kupendwa na watu wengi hata kufikia hatua ya kupokea pongezi kutoka kwa wabungu na  viongozi mbalimbali.

Nay wa mitego anasema kuwa wimbo huo hakumlenga Mh Rais kama watu wengi wanavyosema bali aliamua kutumua tasfida kwa sababu ukiusikiliza kwa makini unakuta kuwa unalenga karibia  kila mtu ambae ni kiongozi katika jamii.

Kikubwa katika hayo, Nay anasema kuwa kitu kikubwa kilichomstua ni baada ya kupokea simu za viongozi wengi lakini pia alipokea simu kutoka BASATA na kama ilivyo ada amekuwa akijua kuwa kama ni  BASATA basi wimbo unaweza kufungiwa kwa muda owowte kutokana na kazi yao kubwa wanayoifanya.

Hata hivyo Nay anasema kuwa safari hii ilikuwa tofauti kwa sababu BASATA walipompigia walikuwa wanampa pongezi za wmbo wak huo.

Tangu nimeachia wimbo huo nimepokea smu nyingi kutoa kwa viongozi weng sana kutoka serikalini wakinipongeza lakini kilichonishtua ni simu kutoka  kwa kiongozi wa BASATA,  na aliniambi kuwa kwake yeye binafsi  hakupiga simu kuzungumiza BASATA bali alipiga simu kunipongeza kwa wimbo huo  kwa kweli nilifurahi sana lakini mpaka sasa sijapokea simu kutoka kwao.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad