Ndoa Ya Dogo Janja na Irene Uwoya Haijavunjika


Msanii wa muzik wa Bongo fleva kutokea Tip Top Connection Kassim Mganga ameibuka na kudai ndoa ya staa wa Bongo fleva Dogo Janja na Mkewe Uwoya haijavunjika.

Kassim Mganga ambaye alikuwa mmoja kati ya watu wachache waliohudhuria ndoa ya Dogo Janja na Uwoya Mwaka jana mwishoni amesema hana taarifa ya ndoa hiyo kuvunjika.

Kwenye moja ya Interview alizofanya hivi Karibuni katika kituo kimoja cha habari Kassim amefunguka na kudai kuwa hajui kama Ndoa hiyo imevunjika kwa kuwa hajapata taarifa Rasmi.

Sina taarifa ya kuvunjika kwa ndoa kati ya Dogo Janja na Irene Uwoya ninachojua bado wako pamoja mpaka hivi sasa”.

Lakini pia Kwenye Mahojiano hayo Kassim amewataka watu wasimuonee wivu Diamond kwa ajili ya mafanikio anayoyapata kwani kiukweli amebadilisha sana muziki wa Bongo fleva.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad