Pretty Kind Achekelea Penzi la Daimond na Mobetto Kuvunjika "Hili ni Fundisho kwa Mobetto Ajue Uchawi Hauna Nguvu Katika Mapenzi''

Pretty Kind Achekelea Penzi la Daimond na Mobetto Kuvunjika "Hili ni Fundisho kwa Mobetto Ajue Uchawi Hauna Nguvu Katika Mapenzi''
SIKU chache baada ya mwanamitindo, Hamisa Mobeto kuanika ukweli kwamba penzi lake na mzazi mwenzake ambaye ni msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ limevunjika, msanii wa filamu na muziki, Suzan Michael ‘Pretty Kind’ amefunguka kufurahishwa na kitendo hicho.



Pretty alisema kwanza anafurahi kwa sababu yaliyotokea ni Mungu kaamua kumuumbua Mobeto kutokana na uchawi aliokuwa anamfanyia Diamond na hilo ni fundisho kwa wasichana wengi wanaoamini uchawi katika mapenzi.



“Kilichomtokea Mobeto ni fundisho kwa wasichana wengi na wanatakiwa kujua kwamba mapenzi hayalazimishwi na kamwe uchawi hauna nguvu katika mapenzi,” alisema Pretty.



Kwa upande mwingine alimtaka Mobeto asihangaike sana kutangaza kuwa ameachana na Diamond huku akiwa bado anamuhitaji pia ajue kwamba hawezi kuolewa na msanii huyo bali yupo mke wa Diamond atakayeolewa hivi karibuni kwake yeye haiwezi kutokea.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad