Rais Mstaafu Mwinyi Atoa Rambi Rambi ya Milioni Mbili Ajali ya MV Nyerere

Rais Mstaafu Mwinyi Atoa RambiRambi ya Milioni Mbili Ajali ya MV Nyerere
Rais Mstaafu wa awamu wa pili, Ali Hassan Mwinyi, ametoa rambirambi ya Sh milioni mbili kwa familia za waliopoteza ndugu zao katika ajali ya kivuko cha Mv Nyerere.

Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wazee duniani yaliyofanyika kitaifa jijini hapa leo Jumatatu Oktoba Mosi, Rais huyo mstaafu aliwaomba wazee na makundi mbalimbali waliohudhuria maadhimisho hayo kusimama kwa dakika moja kwa ajili ya kuwakumbuka waliopoteza maisha katika ajali hiyo iliyotokea hivi karibuni na kuua watu zaidi ya 200.

“Tunakutana hapa baada ya janga kubwa lililotokea Ziwa Victoria, waswahili wanasema mkaa na maiti haachi kulia lia nami naanza kwa kutoa milioni mbili kama rambirambi,” amesema Mwinyi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad