Rich Mavoko Afungukia Bifu Lake na WCB..."Mimi Nilikuwa Brand Kubwa Wakati Naingia WCB"

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Rich Mavoko amefunguka na kuweka wazi uhusiano wake na Label yake ya zamani ya WCB.

Rich Mavoko ameweka wazi kuwa pamoja na kwamba ameondoka katika Label hiyo lakini hana tatizo lolote na CEO wa Label hiyo Diamond Platnumz.

Kwenye Interview aliyofanya na kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Rich amesema kuwa kilichotokea mpaka akaondoka Kwenye Label hiyo sio ugomvi bali muda wa kufanya Biashara ulifikia kikomo hivyo sasa wapo vizuri.

Lakini pia Rich Mavoko amemtaka meneja wa WCB Sallam SK kuwa na busara na heshima ni baada ya Meneja huyo kusema Mavoko hajarudisha hata robo ya pesa waliyowekeza kwake na kumtengeneza kama Brand:

Unajua Kwenye masuala ya kumzungumzia Rich Mavoko unazungumzia Brand ambayo ilikuwepo kwaiyo uliichukua kwa nia ya kufanya nayo biashara sasa umesema hajarudisha sasa na huyo mwenye talent atakuwa amepata?”.

Mavoko aliendelea kutiririka na kumwaga povu zito:

Mimi sitaki kuongelea sana hivi vitu kwa undani kila mtu anatakiwa kuheshimu kitu cha mwenzake ndio tuanze kuongeleana na kuongeleana vitu vibaya ni kutafuta mtu kujitetea”.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad