Sanchi Adai Hakuna Mwanaume Mwenye Hadhia Ya Kuwa Naye Bongo



Socialite maarufu Kwenye mitandao ya kijamii Jane Rimoy maarufu kama Sanchi amefunguka na kudai hajaona mwanaume ambaye anaweza kuwa naye Bongo licha ya kumtongoza sana.

Katika mahojiano yake na gazeti la Amani, Sanchi alisema kuwa kama  kuwa na uhusiano na mwanaume wa Kibongo angefanya hivyo lakini hajaona mwanaume wa kuwa naye na wala hawashobokei kwani kama ni wanaume wamejaa kwenye ukurasa wake wa Instagram ambao humfuata kwa njia ya meseji za moja kwa moja.

Unajua mimi siwezi kuwashobokea kabisa wanaume wa Kibongo kama kunitongoza wamenitongoza sana, si hao tu hata wanaume wa nje tena mastaa Marekani, wanamuziki na wanamichezo wamekuwa wakinisumbua sana na sijawa na uhusiano nao sembuse hao wa Kibongo siwataki“.

Lakini pia Sanchi amefunguka na kujibu maswali ya watu wanaomuhoji kama ametongozwa na msanii mkubwa wa Bongo fleva:

Huyo msanii wao alishanitongoza na nikamkataa, si huyo tu wasanii karibu wote wakubwa Bongo wameshanitaka nikawakatalia, siwataki. Wenye hamu ya kumjua mtu wangu ipo siku nitamuanika”.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad