Steve Nyerere Atoa ya Moyoni Sakata la Video Chafu za Wema-"Amekosea Sana"

Steve Nyerere Atoa ya Moyoni Sakata la Video Chafu za Wema-"Amekosea Sana"
Msanii Steve Nyerere amefunguka na kuongelea swala la Wema kuomba msamaha mbele ya waandishi wa habari baada ya kusambazwa kwa picha zake chafu katika mitandao ya kijamii akiwa faragha na mume wake mtarajiwa.

Steve Nyerere anasema kuwa yeye kama yeye anaamini kuwa Wema amekosea sana na anakubali kuwa waidhalilishwa kwa sababu wao i watu wa karibu na hata yanapotokea mabaya kama hayo wapo wanaokaa na kuwauliza kama wao wanafanya ninikumshauri wema mazuri.

Hata hivyo Steve anasema kuwa pamoja na kwamba amekiri na kuomba msahama lakini akae akijua kuwa kuna vyombo vikuba husika ambavyo vinaweza kukaa na kutafakari kosa lake , madhara yake na ukubwa wa kuomba msamaha wake na yeye hapo hawezi kuingila mamlaka husika.

mimi  sio mhukumu , mimi ni rafiki, kama ndugu wa karibu na jirani yake pia na ninasema kuwa Wema amekosea na amesimama kuomba radhi  lakini kuna vyombo kuna BASATA  kuna TAFF  na kuna wizara pia kama wizara na wao pia wamekaa kimya wanajitafaruku siwezi kuwasemea, lakini kwa upande wangu kweli wema amekosea na ametuomba radhi na ni kweli tulivuliwa nguo , hii ni kwa sababu watu walianza kuhoji kuwa hata wewe haukujamshauri.

Steve nyerere anasema kuwa wasanii wanapaswa kuwa makini sana wanapofanya jambo lolote kutokana na uwepo wa mitandao ambayo kila siku inakuwa na maendeleo ,hivyo kila kitu kinachoongelewa kwa sasa kinabaki mpaka kifo chao na bado yataendelea kuishi miaka na miaka.

lazima ifike muda tujitathmini kwa sababu haya yanayoonekana katika mitandao yanadumu mpaka tunakufa.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad