Yabainika Mfanyabiashara Lugumi Hakuwa na Tatizo ila Serikali


Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema baada ya uchunguzi waligundua kwamba Lugumi hakuwa na kosa ila serikali ndo ilikuwa na matatizo

Kuhusu tenda aliyopewa Said Lugumi ili afunge mashine za utambuzi wa alama za vidole Waziri Lugola amesema utetezi wa Lugumi uko sahihi

Alifunga katika Vituo vya Polisi 32 badala ya 108 kwasababu Serikali haikumuandalia vituo vingine vya kufunga mashine hizo

Akaongeza kuwa masuala mengi kuhusu sakata la Serikali na mfanyabiashara huyo yameripotiwa kinyume

Aidha, Said Lugumi ameeleza kuwa alishindwa kufanya kazi yake vizuri kutokana na kukwamishwa na mkongo wa taifa wa mtandao(Internet)

Source: Jamii Forums
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad