Amber Lulu Arudisha Penzi kwa Prezzo

Amber Lulu Arudisha Penzi kwa Prezzo
Msanii wa muziki Bongo, Amber Lulu ameamua kurudisha mapenzi yake kwa Prezzo.

Amber Lulu amesema kuwa amedharaulika na  kuteseka sana kwenye mapenzi hivyo hana budi kuendelea kuwa na Prezzo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

"Jaman sijazoea kuangaika na niko hivi nikipenda napenda kweli no matter what !! Sasa mnataka kuona kila siku na Bwana mpya, siwez na nishateseka sana nishadharaulika sana. Ni zaidi ya mateso kwenye mapenzi kukanwa kupigwa nishakuwa kama mtumwa nishapata stress mpaka napoteza nuru.

"Nikawa naonekana kama teja kwa huyu hakuna hivyo vitu ananijali anajuwa maana ya upendo ananiheshimu, nyie mnaniona kicheche yeye ananiona qeen Elizabeth na matatizo yangu hajawai hata kunidharau anajuwa thamani yangu kwanini nisirudi kwake niacheni jamani."

Muimbaji huyo ameshawahi kutoka kimapenzi na waimbaji kadhaa wa Bongo Fleva kama Barnaba,Young Dee na Aslay.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad