Faiza Ally Awatolea Povu Zito Wanaotaka Kuongeza Makalio Kwa Madawa


Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu kwenye mitandao ya kijamii Faiza Ally amejikutwa akiwatolea Povu Zito wanawake ambao wamekuwa wakimsumbua kuhusu madawa ya kuongeza makalio.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Faiza aliweka wazi kuwa kuna wanawake wamekuwa wakimsumbua kwa kutaka kumtuma madawa ya kichina ya kuongeza makalio.



Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Faiza ambaye pia ni mfanyabiashara alisema hakuna jambo ambalo halipendi kama mtu kumuagiza dawa za kufanya mabadiliko kwenye mwili hivyo anawasihi wanawake wajikubali kama walivyoumbwa.

Sipendi wanawake kutojikubali. Mimi siwezi kumletea mtu dawa ya kuongeza makalio maana naona kama si za kweli, lakini pia ni vyema kujikubali, hicho ndicho kitu muhimu“.

Faiza ambaye hivi sasa yupo nchini China kwa ajili ya kufunga mizigo ya wateja alianika meseji za wanawake ambao wanaomba kuletewa madawa ya kuomgeza hipsi na makalio.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad