Lava Lava Afungukia Tuhuma Za Kumtelekeza Mwanamke Mjamzito


Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka katika kundi la WCB Abdul Iddi maarufu kama Lava Lava amefunguka na kukana kabisa tetesi zilizosambaa kuwa ametelekeza mwanamke wake ambaye ni mjamzito.

Lava Lava amekana Tetesi hizo ambazo zimekuwa zikisikika kwenye Social media na kudai hazina Ukweli wowote lakini pia amedai anashukuru kwa Baraka ya kupewa mtoto hewa.

Katika mahojiano yake na Global Publishers, Lava Lava alisema uvumi huo hata yeye alisikia na kuona baadhi ya video ambazo zilivujishwa kama ushahidi juu ya uhusiano wake na mwanamke huyo akidai kuwa ana mimba yake, lakini hata hamfahamu.

Niliwahi kutumiwa meseji nyingi na mojawapo ni ya mwanamke huyo ambaye yupo nyumbani tu hafanyi muziki ila alikuwa anataka kuwa staa tu, aliniambia anataka kufanya kiki na mimi awe staa nisimchukulie vibaya, nikaisoma na kuiacha“.

Wasanii kadhaa wamekuwa wakisingiziwa hata kutengeneza wenyewe skendo Kama hizi ili kuweza kuongeza umaarufu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad