Madereva Wagoma Bukoba, Polisi waibuka

Madereva Wagoma Bukoba, Polisi waibuka
Kamanda wa Polisi Bukoba, Revocatus Malimi amesema jeshi hilo linafuatilia mgomo wa madereva uliotokea kwenye manispaa hiyo kwa kile kilichodaiwa ni kupinga baadhi ya tozo zilizowekwa na manispaa hiyo.

Kwa mujibu wa Kamanda Malimi, Jeshi la Polisi linafuatilia kwa ukaribu ili kufahamu kuwa waliogoma ni madereva au ni wamiliki wa magari, na hivi karibuni jeshi hilo litatoa taarifa juu ya mgomo huo.

Akizungumza na www.eatv.tv Kamanda Revocatus Malimi amesema “taarifa ni za kweli ila jeshi letu linafuatilia lijue madai yao ni nini, pia tunahitaji kujua waliogoma ni wasafirishaji au ni abiria, na tumeambiwa ni mgomo baridi wa kutokutoa huduma.”

Mapema leo majira ya saa 3 asubuhi zilianza kusambaa taarifa juu ya kutokea kwa mgomo wa madereva wa daladala kutokutoa huduma za usafiri wakielekeza malalamiko yao kwa manispaa ya Bukoba.

Mbali na madai hayo pia inaelezwa kuwa madereva hao pia wanagomea juu ya ubovu wa miundombinu kwenye eneo ambalo wamekuwa wakiegesha magari yao.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad