Msuva 'Tupo Tayari Kupambana Bila ya Mbwana Samatta'


Stars itamkosa nahodha wake @samagoal77 katika mchezo wa kesho ambaye anatumikia adhabu ya kadi za njano, @msuva27 anasema, kukosekana kwake kunawapa morali na watapambana zaidi kwa lengo la kufuzu fainali za mataifa ya Afrika.

"Samatta ni mchezaji muhimu kwetu, mchezani ambaye anatupa sapoti kama wachezaji pia ni mzoefu. Tunamkosa lakini sisi wachezaji wenzake tumeweka nguvu na yeye ametuambia anaamini katika mechi hii tutafanya vizuri kwa sababu anaamini tutapambana"-Msuva.

"Tuko tayari kupambana kwenye mechi hii kwa sababu tunahitaji kufika hatua ambayo kila mtu  anahitaji sisi tufike. Kila mchezaji anatamani kufika AFCON hilo ndio lengo letu kubwa."
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad