Mtibwa Sugar Waziita Timu za Simba na Yanga

Mtibwa Sugar Waziita Timu za Simba na Yanga
Uongozi wa timu ya Mtibwa Sugar, umesema kuwa umewaita viongozi wa Simba na Yanga ili waweze kuwaunga mkono katika mashindano ya kimataifa.

Ofisa habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru amesema  watacheza na washelisheli siku ya jumanne majira ya saa 10:00 jioni uwanja wa Chamazi jijini Dar es Salaam.

"Timu mbili Simba na Mtibwa zinawakilisha Taifa kimataifa hivyo ni jukumu letu watanzania kuungana na kuwa kitu kimoja.

"Nimewaalika ndugu zangu wa Simba, Yanga, na Ruvu Shooting na timu zote kwa pamoja tuungane kupeperusha bendera yetu, watanzania wote tushirikiane," alisema.

Mtibwa Sugar wanawakilisha taifa kwenye Michuano ya Kombe Shirikisho ambapo Jumanne wataanza kupeperusha bendera kwa kucheza na Northern Dynamo kutoka Shelisheli.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad