Mtoto Aokotwa Akiwa Amefariki Katika Mtaa wa Sido Mkoani Njombe


Mtoto anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 2-3 ambaye hajajulikana jina lake amekutwa ametupwa korongoni karibu na Msitu uliopo pembezoni mwa kanisa la EAGT

Mtendaji wa Mtaa, Rehema Ngailo amesema alipata taarifa ya kuonekana kwa mwili huo mapema asubuhi ya leo na kuijulisha Polisi

Amesema "Tumesambaza taarifa kwa Wananchi kuangalia kila nyumba kama kuna mtu aliyekuwa na mtoto na sasa hana ili tupeane taarifa na kumtambua aliyehusika"

Wiki mbili zilizopita mtoto mwingine mchanga aliokotwa katika dampo la Kipagamo mjini Makambako akiwa hai na kupelekwa kituo cha kulelea watoto cha Tumaini Ilunda

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad