Mzee Yusuph Aombea Dua Mziki wa Taarabu ufe

Aliyekuwa msanii wa muziki wa taarabu nchini Tanzania, Alhaji Mzee Yusuph Mwinyi amesema kuwa hajui kama taarabu imeyumba kwasababu hajapata nafasi ya kusikiliza.

Alhaji Mzee Yusuph amesema kuwa kama taarabu inayumba ataomba dua ianguke na watu watafute vitu vizuri zaidi.

"Siijui na siisikilizi yaani sijapata nafasi ya kuusikiliza na sitaki kabisa kujua kunaendeleaje kama kuna yumba ntaomba dua zaidi kuanguke kusiyumbe, watafute vitu vizuri zaidi ya taarabu ," alisema Mzee Yusuph katika mahojiano yake na Azam Tv.

"Nimeacha taarabu wakati bado napenda unaelewa huyo kuacha wakati unapenda na nikamuomba Allah nikamwambia napenda hiki kitu lakini nakiacha, sasa nijaalie nikichukie maana yake nimeacha kitu ambapo bado kinaendelea kufanya maisha."

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad