Noti za Tanzania ni Chafu Sana, BOT iingilie Kati na Kutoa Elimu ya Utunzaji


Mdau wa JamiiForums anasema amewahi kudhani kuwa fedha na sarafu za Tanzania zinatengenezwa kwa ubora wa kiwango duni na zinaachwa kwenye mzunguko kwa muda mrefu

Anasema kuwa Watanzania wanakunja noti bila ya mpangilio, noti zinahifadhiwa kwenye vifua(Wanawake) na wengi hawatumii 'pochi' kuhifadhi fedha

Kuna wafanyabiashara wanashika fedha huku wakiwa na mikono michafu mfano, wauza vimiminika kama mafuta, nyama, nafaka na Mkaa

Madhara ya uchafuzi huu ni makubwa kwani noti zinachakaa na kuilazimisha Serikali kuingia gharama za kuchapicha noti mpya

Mdau anaishauri Benki Kuu(BoT) ifanye mkakati wa kutoa elimu kwa umma juu ya njia bora ya kuhifadhi fedha na sarafu
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad