RC Makonda Afunguka Kilichomsababisha Kumwaga Chozi Kanisani

RC Makonda Afunguka Kilichomsababisha Kumwaga Chozi Kanisani
Siku moja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kutokwa na machozi akiwa katika ibada katika kanisa la Efatha linaloongozwa na mtumishi wa Mungu Josephat Mwingira kiongozi huyo ameibuka na kutoa neno.


Kupitia ukurasa wake wa Instagram Makonda amechapisha video ambayo alionekana akiwa na anatokwa na machozi kanisani hapo na kuandika ujumbe ambao alibainisha watu wengi hawajui kilichotokea.

Makonda ameandika “Powerful, very powerful watu hawaelewi nini kimefanyika Ila mbinguni wameelewa na wameandika, people think it’s a joke. Ila kwa Mungu hakuna mzaha, asante Mungu Kwa kusimama upande wangu”

Hivi karibuni Mkuu wa huyo wa Mkoa Dar es salaam alianzisha kampeni maalum ya kuwakamata watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, na kuunda kamati maalum ya watu 17 ili ya kushughulika na suala hilo.

Jana kupitia ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje, ilisema zoezi linaloendeshwa na Mkuu wa Mkoa wa ni mawazo yake binafsi na si msimamo wa serikali.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad