Rc Makonda Afunguka Ukaribu Wake na Ruge Ahaidi Kushiriki Fiesta Dar "Alinitungia Wimbo Maalum Kwaajili ya Mwanangu Keagan"

Rc Makonda Afunguka Ukaribu Wake na Ruge Ahaidi Kushiriki Fiesta Dar "Alinitungia Wimbo Maalum Kwaajili ya Mwanangu Keagan"
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Mhe. Paul Makonda amethibitisha kuwa hata yeye atahudhuria kwenye fainali ya Tamasha la Tigo Fiesta, itakayofanyika katika viwanja vya Leaders Jumamosi hii.


RC Makonda akizungumzia tamasha hilo,  pia ameelezea mahusiano yake kwa sasa na Boss wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba ambapo amesema wamekuwa karibu kama mtu na kaka yake.

Ruge ni kaka yangu, na nikwambie hivyo nilivyompata Keagan (mtoto wa RC makonda) ametunga wimbo maalumu kwa ajili ya Keagan. Unafahamu kama alivyokuwa India (Kwenye matibabu)  Mimi nilikuwa na wasiliana nae?. Unafahamu kuwa alishawahi kuja nyumbani kumuona mtoto?. Unafahamu kuwa alishawahi kuja nyumbani kwa ajili ya maombi? Ruge ana watoto… Fiesta nitakuwepo na itakuwa kubwa kuliko,”amesema RC Makonda.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad