Shilole Awatahadharisha Watu Wanaomuiga Biashara Zake

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole ameibuka na kuwataka somo kali mastaa wenzake ambao wamekuwa wakijiingiza katika biashara za kupika.

Shilole ni mmoja kati ya wasanii ambaye pamoja kuimba Lakini pia ni mjasiriamali kwani anamiliki mgahawa unaojulikana kama Shishi Food ambao unafanya vizuri sana hapa mjini.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Amani, Shilole alisema anafurahi kuona kile alichoanzisha kinaigwa na wasanii wenzake wengi ila tahadhari ni kwamba wanatakiwa kukomaa sana kwani vitu vya kuiga bila kuwa na misingi imara watashindwa.

Ni sawa wameniiga wengi lakini wanatakiwa kuwa na misingi imara vinginevyo wataanguka, nimekuwa mfano wa kuigwa kwa sababu mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kuanzisha mama lishe kwa kufungua mgahawa ndiyo wengine wakafuata hivyo watambue kuwa aliyeanza kaanza tu, niko kwenye biashara hii kwa miaka mitatu sasa hivyo naamini hakuna wa kunishinda“.

Mastaa wambao pia wanatajwa kuanzisha biashara ya mgahawa Baada ya Shilole ni pamoja na msanii wa Bongo movie Esha Buheti.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Upo maeneo gani mgahawa wako Dada ili nije nitakapokuwa dar. Nimependa presentation yako

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad