Tekno Hali Tete Akubwa na Ugonjwa la Ajabu

Tekno Hali Tete Akubwa na Gonjwa la Ajabu
Uongozi wa msanii wa muziki nchini Nigeria, Tekno Miles, umewataka mashabiki kumuombea msanii huyo kutokana na ugonjwa unaomsumbua, ambao utamuhitaji kukaa nje ya muziki kwa muda.


Kwenye ukurasa wa instagram wa Mr. Ubi Franklin ambaye ni CEO wa kampuni inayomsimamia Tekno, umewekwa post inayotoa taarifa rasmi juu ya hali ya msanii huyo, na kuutaarifu umma kuwa kwa sasa hatofanya kazi za muziki ili kupata matibabu zaidi na kujipa muda wa kupona.

'Post' hiyo imesema kwamba kwa muda wa miezi miwili ilikuwa migumu kwa msanii Tekno kutokana na ugonjwa uliokuwa ukimsumbua ambao mwenyewe aliamini utaisha baada ya muda, lakini kutokana na hali yake kuwa si nzuri madaktari wameshauri asifanye kazi za muziki, ili aweze kupona zaidi.

Uongozi huo ulienda mbali zaidi kwa kusema kuwa Tekno amepata hitilafu kwenye mfumo wake wa saut kutokana na kuchoka kwa kazi nyingi na kuperform mara kwa mara, lakini atakuwa sawa na kazi zitaendelea kama kawaida.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad