Baada ya Kunyakua Tuzo Calisah Aitupia Lawama Serikali

Baada ya Kunyakua Tuzo Calisah Aitupia Lawama Serikali
BAADA ya kufanikiwa kuiwakilisha vyema Tanzania na kuwa mshindi wa Mr Africa International 2018, huko nchini Nigeria mwanamitindo, Calisah Abdulhamiid ameelezea furaha aliyonayo kwa sasa kwa kuwashukuru Watanzania wote waliompigia kura na kuilalamikia Serikali kutompa sapoti katika safari yake ya kuelekea nchini humo. 



Calisah aliibuka mshindi wa Mr Africa huko nchini Nigeria Desemba 2. Akizungumza na Ijumaa Calisah alisema;

“Kwa kweli nilifarijika sana baada ya kutangazwa kuwa mimi ndio mshindi, licha ya kwamba kabla ya safari yangu ya kuelekea Nigeria nilipitia changamoto nyingi ikiwemo kutopata ushirikiano kabisa toka kwa Serikali yangu, kwa sababu hata bendera niliyoitumia niliishona mwenyewe kwa fundi, hivyo nimepata tabu sana mpaka kufikia hapa,” alisema Calisah.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad