Basata Yakanusha Kuwafungulia Daimond na Rayvanny Kufanya Shoo

Basata Yakanusha Kuwafungulia Daimond na Rayvanny Kufanya Shoo
Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) nchini Tanzania limekanusha kuwafungulia wasanii Diamond Platnumz na Rayvanny wanaotumikia adhabu ya kutojihusisha na sanaa kwa muda usiojulikana baada ya kufanya makosa mbalimbali ndani ya kipindi cha miezi miwili.

Taarifa ya Naibu Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Onesmo Kayanda iliyotolewa leo Jumamosi Desemba 22, 2018 imesema haijawaondolea adhabu hiyo na kuwakata wafuate maagizo waliyopewa ikiwamo kutofanya maonyesho nje ya nchi.

Jana, wasanii hao kupitia mtandao wa Instagram waliomba radhi kwa mamlaka mbalimbali nchini na jioni walionekana wakifanya mkutano na wanahabari nchini Kenya kutangaza maonyesho yao yanayoendelea.

"Ikumbukwe kuwa Desemba 18 tuliwafungia kutojihusisha na sanaa kwa kipindi kisichojulikana kwa kuimba kwa makusudi wimbo Mwanza tulioufungia kwa sababu za kimaadili,

"Baraza linasisitiza kuwa halijawafungulia wasanii hao, pia linawaonya kuacha kutoa taarifa za uongo kabla halijawachukulia hatua kali zaidi," imesema taarifa hiyo ya Kayanda.

Diamond na Rayvanny wameingia matatani wakituhumiwa kufanya makosa mbalimbali ikiwamo la kutumbuiza wimbo uliofungiwa, kufanya tamasha mkoani Mwanza bila kibali, kutoa lugha ya matusi jukwaani mkoani Mtwara na kutofuata taratibu za usajili wa matamasha.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad