CCM Yaahidi Kuendelea Kutekeleza Ahadi, Yafanya Jambo hili Dar


CHAMA Cha Mapinduzi  (CCM) kimesema kitaendelea  kusimamia kikamilifu  utekelezaji wa Ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2015/20, ikiwa ni katika kutoa huduma bora kwa wananchi likiwemo kundi la watu wenye mahitaji maalumu.

Hayoyalisemwa na Mjumbe wa Halmshauri Kuu ya CCM (NEC), Mkoa wa Dar es  Salaam,  Yusuph Nassor , wakati akikabidhi msaada wa bidhaa mbalimbali  katika kituo cha  kulelea watu wenye mahitaji maalumu cha Cha Mission of Charity , Mburahati, Wilayani Ubungo,

Kituo hicho kina lea watu  wenye mahitaji maalimu zaidi ya  100 wakiwemo, watoto waliotupwa au kutelekezwa baada ya kuzaliwa, wenye ulemavu, wazee na masikini.

“Dhamira ya CCM ni kuhakikisha  wananchi wanapata huduma zote muhimu. Lakini pia kusaidia watu wenye mahitaji maalumu. Chama kimeamua  kutoa msaada wa chakula, sabuni na mahitaji mengine katika kituo hiki,”alisema Nassor.

Alitoa wito kwa wadau wengine hususan serikali kuendelea kuhudumia kituo hicho  ambacho kina mahitaji mengi.

Sambamba nahilo mjumbe huyo wa NEC,  aliitaka  jumuiya za wazazi , UWT,na vijana, kusimamia kikamilifu suala la maadili katikajamii.

“Jumuia hizi za Chama ndiyo   zinajukumu kubwa la kusimamia suala zima la maadili  katika jamii ambayo hivi karibuni yamekuwa yanayumbayumba,’alisema.

Akipokea msaada huo  Kiongozi wa Huduma  wa Kituo cha Mission of Charity Sista  Lily Thomas, aliishukuru CCM hususan kata ya Mburahati kwa misaada hiyo.

Naye  Sister Maria Joseph, alisema, miongoni mwa changamoto kubwa  inayo kikabili kituo ni ubovu wa barabara inayo ingia kituo hapo pamoja na  miundombinu ya kupitishia maji machafu ambayo wakati wa kiangazi inaziba  na kutapisha maji  hayo katika kitu.

Mwenyekiti wa  Jumuiya ya wazazi  CCM kata ya  Mburahati, John Exavery Mapunda alisema, Chama kitaendelea kusaidia kuwa karibu na kituo hicho ili kusaidia  mahitaji mbalimbali ya msingi.

“Mbali na hilo, alisema Chama kimejipanga  kikamilifu kuhakikisha  kinaibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa serikali za mtaa unaotarajiwa kufanyika mapema mwakani,”alisema Mapunda..

Pamoja na hayo, Jumuia ya Wazazi Kata ya Mburahati iliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani kwa mwaka 2018 mbele ya kikao cha Bara la  Wazazi, na Wanachama na kumpongeza Mwenyekiti Rais Dk. John Magufuli kwa kasi kubwa ya utekelezaji wa ilani.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad