CCM Yawasamehe Na Kuwarejeshea Uanachama Ramadhani Madabida Na Wenzake Watatu


CCM Yawasamehe Na Kuwarejeshea Uanachama Ramadhani Madabida Na Wenzake Watatu
Kwa kauli moja Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imepokea maombi na kukubali kusamehewa adhabu ya kufukuzwa uanachama kutoka kwa waliokuwa wana CCM wanne ambao walitenda makosa hayo wakiwa Wenyeviti wa CCM ngazi ya Mikoa na Wilaya.


Waliosamehewa na kurejeshewa uanachama ni;

1. Ndg. Ramadhani Rashid Madabida (aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam).

2. Ndg. Erasto Izengo Kwirasa (aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga).

3. Ndg. Christopher Mwita Sanya (aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara).

4. Ndg. Salum Kondo Madenge (aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni).

Wanachama hao waliosamehewa wakimshukuru Mwenyekiti wa CCM Dkt. Magufuli, Makamu Mwenyekiti, Philip Mangula na Katibu Mkuu Dkt. Bashiru Ally mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC) wakati wa Kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa leo tarehe Desemba 18, 2018 Jijini Dar es Salaam

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad